Tuesday 6 October 2015

NIMEIINGIA BUMBULI LEO KUZUNGUMZA NA WANANCHI,CHAGUO LAO CCM ,CHAGUO LAO JANUARY MAKAMBA KWA BUMBULI

Mwigulu Nchemba na Mbunge mtarajiwa wa Jimbo la Bumbuli Mh.January Makamba wakiwasili Kata ya Usambara kwaajili ya Mkutano wa hadhara wa kampeni mapema hii leo.Wajumbe wa timu ya Kampeni ya Ushindi ya Chama cha Mapinduzi wakiteta Jambo.January Makamba akimsikiliza Mwananchi wake kwa Makini.Mwigulu Nchemba akizungumza na Wananchi wa kata ya Funta hii leo.Mwigulu Nchemba akizungumza na Wananchi wa kata ya Tamota wakati wa kuomba kura za Urais,Ubunge na Udiwani kwa Chama cha Mapinduzi hii leo Jimbo la Bumbuli.January Makamba akizungumza na Wananchi wake namna alivyotekeleza ahadi zake zilizopita na anavyokwenda kusimamia ilani ya Uchaguzi kwa miaka 5 ijayo kwa wananchi wa kata ya Tamota.Moja ya jambo kubwa la kimaendeleo kwa kata ya Tamota ni kupata umeme uliofika makao makuu ya kata hiyo.,January Makamba akizungumza na Wananchi wake wa Vuga,Mbali na kuwaomba kufanya uchaguzi kwa Amani,Pia amesisitiza Watumishi wa serikali kuacha kujihusisha na siasa chafu,Wazingatie maadili ya kazi zao ilikuijenga Tanzania imara.Wananchi wa kata ya Vuga wakishangilia Utekelezaji wa shughuli za maendeleo uliokuwa ukitajwa na Mbunge wao Januray Makamba.Mwigulu Nchemba na January Makamba wakiaganana Wananchi wa kata ya Fuga mra baada ya Mkutano wa hadhara wa kampeni.January Makamba akisikiliza hoja za Wananchi wake kuhusu Maendeleo ya Bumbuli.Mwigulu NChemba na January Makamba wakiwasili kata ya Mbonde.Mapokezi yakiendelea..Mbunge Mtarajiwa wa Jimbo la Bumbuli.Mwigulu Nchemba akimnadi January Makamba kwa Wananchi wa kata ya Mbonde,Amesisitiza kuwa Bumbuli ni Halmashauri mpya ambayo imepatikana kwajitihada za Mbunge January Makamba hivyo wamuache aimarishe Halmashauri hiyo ,Pia ameahidi kusaidiana na January Makamba kuhakikisha Kiwanda cha Chai kinafunguliwa haraka iwezekanavyo katika kata hiyo.Mwigulu Nchemba akizungumza na Wananchi wa Mbonde hapa Bumbuli hii leo.January Makamba akizungumza na wananchiwa Mbonde kuwa ahadi yake kubwa atakayohakikisha inafanyiwa kazi ndani ya muda mfupi ni Ufunguzi wa kiwanda cha Chai kata ya Mbonde ilikurejesha shughuli za Uchumi za Wananchi wa Bumbuli zinazotokana na zao la Chai.Mwigulu Nchemba akiagana na Wananchi wakata ya Mponde.Vijana wa kazi wa Chama cha Mapinduzi wakiwasili kwenye Mkutano wa hadhara Jimbo la Bumbuli hii leo.Mwigulu Nchemba na January Makmba Mbunge wa Bumbuli wakiwasili kwenye Uwanja wa Mkutano Kata ya Soni.January Makamba akisalimiana na Wananchi wake wa kata ya Soni.
Mwigulu Nchemba akizungumza na Wananchi wa kata ya Soni Jimbo la Bumbuli Jioni ya leo.
Umoja wa Wananchi wa kata ya Soni kwa Chama cha Mapinduzi.Mbunge mtarajiwa wa Jimbo la Bumbuli Ndg.January Makamba akizungumza na Wananchi wa kata ya Soni kuhusu Umuhimu wao wa kuendelea kuiamini CCM na kuichagua Kwenye Uchaguzi Mkuu ujao.Mwananchi anapofurahia orodha ya shughuli za Maendeleo alizofanya Mbunge wake January Makamba ikiwa ni pamoja na Kusambaza Umme,Huduma za AFya na kuboresha huduma za Usafiri.Mwigulu Nchemba akimnadi na kumuombea Kura January Makamba kwa Wananchi wa Bumbuli hii leo.January Makamba For Bumbuli.
Picha na Sanga Festo Jr.

No comments:

Post a Comment