Tuesday 4 October 2016

TASIWRA,ZIARA YA MH:MWIGULU NCHEMBA ALIYOIFANYA UNGUJA HII LEO

 Waziri wa Mambo ya ndani ya nchi Mh:Mwigulu Nchemba akikagua gwaride la askari mara baada ya kuwasili makao makuu ya jeshi la polisi zanzibar.
 Mapokezi yakiendelea kwa waziri wa mambo ya ndani ya nchi mara baada ya kuwasili kisiwani Unguja hii leo.
 Mwigulu Nchemba akipokea salamu ya utii kutoka kwa askari wa jeshi la polisi hii leo zanzibar.
 Mwigulu akisalimiana na baadhi ya viongozi wa jeshi la polisi waliopo visiwani Zanzibar.
 Waziri wa mambo ya ndani ya nchi akiongoza kikao cha ndani kilichohusisha viongozi wa juu wa jeshi la polisi Zanzibar.
 Mh:Mwigulu Nchemba akikagua moja ya majengo chakavu yanayohitaji ukarabati ndani ya eneo la Makao makuu ya jeshi la polisi Unguja.
 Waziri wa Mambo ya ndani ya Nchi akiwasili ofisi za Uhamiaji-Zanzibar hii leo.
 Mmoja wa maofisa wa idara ya Uhamiaji akitoa maelezo kwa Waziri Mwigulu Nchemba namna mchakato wa utoaji wa Vitabu vya kusafiria "Passport" vinavyotelewa katika ofisi hiyo.

 Waziri wa mambo ya ndani akiongoza kikao cha watendaji wa idara ya Uhamiaji visiwani Zanzibar hii leo,
 Waziri wa mambo ya ndani katika picha ya pamoja na maafisa wa juu wa idara ya Uhamiaji-Zanzibar.
 Mh:Mwigulu Nchemba akiwa katika picha ya pamoja na watumishiwa idara ya Vitambulisho vya Taifa-NIDA -Zanzibar.
 Mwigulu Nchemba akizungumza na watumishi wa jeshi la polisi,NIDA na Uhamiaji katika Bwalo la polisi-Ziwani hii leo.
Katika mengi aliyozungumza nao,Mh:Mwigulu amesisitiza kuongeza nguvu katika mapambano dhidi ya biashara haramu ya madawa ya kulevya hasa katika usafirishaji majini na maeneo wanayouzia madawa hayo.
 Pia,Mwigulu Nchemba ameweka bayana kuwa ni lazima jeshi la polisi lifanye kazi kwa umoja wa hali ya juu ilikuhakikisha ulinzi na usalama unaendelea kuimarisha nyakati zote.
 Katika hatua nyingine,Waziri wa mambo ya ndani ametoa fursa kwa watumishi wa wa wizara anayoiongoza kutoa kero,changamoto au maoni ambayo yangetumika kuboresha utendaji wa idara anazoiongeza.Katika kero kubwa ambazo askari wameendelea kusisitiza ni makazi na maslahi na malimbikizo ya madeni ya uhamisho na upandshaji wa vyeo kwa wakati.
 Mmoja wa afisa wa idara ya mambo ya ndani akichangia maoni yake na kero zinazopaswa kurekebishwa ilikupambana na wahamiaji haramu katika mipaka ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 Mh:Turky ambaye ni Mbunge wa moja ya jimbo kisiwani Unguja akitoa neno la shukrani kwa waziri kwa namna alivyojitoa kuhakikisha anatatua kero za askari na watumishi wote wa wizara ya mambo ya ndani.
Mwisho,Waziri wa mambo ya ndani amekutana na askari wa jeshi la polisi waliostaafu kwaajili ya kusikiliza ushauri wao katika kuimarisha utendaji kazi wa idara za mambo ya ndani.
Pciha/Maelezo na Festo Sanga Jr.

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI MH:MWIGULU NCHEMBA AKUTANA NA RAIS WA ZANZIBAR MH:DK.ALI MOHAMED SHEIN

Mh:Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akimkaribisha Waziri wa mambo ya ndani ya Nchi Mh:Mwigulu Lameck Nchemba hii leo Ikulu-Zanzibar alipomtembelea kwaajili ya mazungumzo.
 Waziri wa Mambo ya ndani ya Nchi.Mh:Mwigulu Nchemba akifanya mazungumzo na Mh:Rais wa Zanzibar kabla ya kuanza ziara ya kikazi visiwani humo iliyolenga kukutana na vikosi vya jeshi la polisi,NIDA,Uhamiaji n.k.
Wakiagana mara baada ya Mazungumzo.
Picha/Maelezo na Festo Sanga Jr.

Wednesday 10 August 2016

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI,ATEMBELEA KAMBI TATU ZA WAKIMBIZI MKOANI KIGOMA


Waziri wa Mambo ya ndani ya nchi,Mh:Mwigulu Nchemba akiwa na Mkuu wa wilaya wa Buhigwe(Kushoto) Col.Martin Gaguti na Mkuu wa wilaya wa Kasulu Col.Mkisi alipowasili mkoani Kigoma kwa ziara ya kikazi.Kikao cha askari wa magereza,zimamoto,polisi na uhamiaji kikiendelea wakati Mh:Mwigulu nchemba alipokutana nao kwaajili ya kuwaleza dira ya wizara yao na changamto ilizopanga kuzitatua.Mwigulu Nchemba akipewa maelezo kuhusu idadi ya wakimbizi waliopokelewa tangu kuanza kwa mwaka huu wakitokea Burundi.Ambapo kwa takwimu za awali kuna wakimbizi zaidi ya laki moja mkoani kigoma waliowekwa kwenye makambi matatu tofauti.Waziri wa mambo ya ndani akisalimiana na mmoja ya wakimbizi waliopo kwenye kituo kidogo cha Kigoma mjini wakisubiri safari ya kuelekea nchini Marekani na Sweeden kwaajili ya hifadhi.Mwigulu Nchemba akifurahia jambo na wakimbizi wanaoandaliwa kwaajili ya safari ya nje ya nchi kwaajili ya hifadhi.Mkuu wa wilaya ya Buhigwe Col.Martin Gaguti akimpatia maelezo mbalimbali Waziri wa mambo ya ndani alipowasili kwenye mpaka wa manyovu unaotenganisha Tanzania na Burundi.Changamoto ya wakimbizi kutoroka na kurudi nchini kwao kinyemelea,inawafikisha mikononi mwa Mh:Mwigulu Nchemba ambaye ameshuhudia wakimbizi kadhaa katika mpaka wa Manyovu wakijaribu kurejea Burundi kinyemela bila kufuata taratibu.Mwigulu Nchemba alipowasili wilaya ya Kasulu na kupokelewa na Mkuu wa wilaya Col.Mkisi
Katika hatua nyingine,Mwigulu nchemba alilazimika kukutana na madiwani waliopo wilaya ya kasulu kwaajili ya kuwapa somo na angalizo namna ya kusaidia serikali kukamata wahalifu na wakimbizi haramu wanaotishia usalama wa mkoa wa Kigoma.Hawa ni wakimbizi kutoka nchi jirani ya Congo,hapa wapotayari kwaajili ya kusafirishwa kupelekwa Kigoma kwaajili ya usaili wa kusafirishwa kwenda nchi za Ulaya.Mwigulu Nchemba akiagana na wakimbizi wa Congo kwenye kambi ya Nyarugusu.Akiwa katika kambi ya Nyarugusu,Mh:Mwigulu Nchemba akatembelea wodi ya wazazi kwaajili ya kukagua huduma za afya.Hapa waziri Nchemba amempakata mmoja wa watoto wa wakambizi aliyezaliwa katika Hospitali hiyo iliyopo ndani ya kambi.Mwigulu Nchemba akimsalimia mmoja ya watoto waliozaliwa kwenye kambi ya Nyarugusu.Mh:Mwigulu Nchemba akizungumza na watoto ambao ni wakimbizi waliopo katika kambi ya Nyarugusu -Mkoani Kigoma.Mwigulu Nchemba akisaidia ufyatuaji wa tofali za ujenzi wa makazi ya wakimbizi waliomba hifadhi kwenye kambi ya Nduta wilaya ya Kibondo.Moja ya nyumba za kuhifadhi wakimbizi kwa muda zinazoendelea kujengwa kwenye kambi ya Nduta .Msimamizi(Kushoto )wa shughuli za Shirika la wakimbizi Duniani akitoa maelezo kwa Waziri wa mambo ya ndani namna wanavyojitahidi kuhakikisha mazingira ya wakimbizi katika kambi zote tatu wanapata huduma zote muhimu.Waziri wa mambo ya ndani akizungumza na kamati ya Usalama ya wilaya ya Kakonko alipotembelea kambi ya wakimbizi ya Mtendeli.
Picha/Maelezo na Festo Sanga Jr.

Tuesday 9 August 2016

MWIGULU NCHEMBA ALIPOWAVAA WACHINA WATESAJI HUKO GEITA


MWIGULU NCHEMBA ATOA ONYO KALI KWA WAKIMBIZI WANAOFANYA UHALIFU NA UBAGUZI MKOANI KATAVI

Waziri wa Mambo ya ndani akisikiliza ripoti ya Mkoa wa Katavi kutoka kwa kaimu Mkuu wa Mkoa huyo ambaye ni Mkuu wa wilaya ya Mpanda.Askari wa Jeshi la polisi kwa idara zote wakiimba wimbo wa maadili tayari kwa kumsikiliza Mh:Mwigulu Nchemba wilaya ya Mpanda Mjini.Waziri wa mambo ya ndani akiangalia tofali zilizoandaliwa kwaajili ya ujenzi wa makazi ya askari mpanda mjini.Kamati ya Usalama wa Mkoa wa Katavi wakimuonesha Mh:Mwigulu Nchemba sehemu iliyobakia katika ujenzi wa ukumbi wa mikutano wa jeshi la polisi.Mwigulu amepongeza hatua hizo na kuahidi kuhakikisha anawasaidia kukamilisha hatua iliyobakia haraka iwezekanavyo.Mwigulu Nchemba akiwasili kwenye Gereza la mpanda kwaajili ya kusikiliza kero za wafungwa.Mwigulu Nchemba akiwasili ofisi za UNHCR zilizopo Shimano umbali wa KM 200 kutoka Kigoma Mjini.Mwigulu akipata maelekezo kutoka kwa Mkuu wa Makazi wa kambi ya Katumba alipotembelea kukagua uhakiki wa wakimbizi unaoendelea katika kambi hiyo.Mwigulu akiondoka kambi ya Katumba mkoani Katavi."Nyumba ya askari inapaswa kuwa na hadhi kama hii,uwezo tuna na nia tunayo ya kuhakikisha askari wetu wanakaa kwenye makazi bora"Mwigulu Nchemba akitoka kukagua nyumba ya kisasa kukaa askari polisi katika wilaya pendekezwa ya Tanganyika.Nyumba imejengwa kwa ushirikiano kati ya wananchi,UNHCR na Serikali ya Tanzania.
Waziri wa mambo ya ndani ya Nchi,Mh:Mwigulu Nchemba akiagana na wakimbizi waliopo kambi ya Shimano iliyopo Mkoa wa Rukwa mara baada ya kuzungumza nao.

Katika ziara yake kwenye kambi ya wakimbizi ya Katumba na Shimano,Mwigulu Nchemba amezungumza na wakimbizi hao ambao wale wa Katumba walipewa Uraia mwaka 2009 na wa Shimano bado hawajapewa Uraia.Akizungumza nao katika hali ya kusikitisha,kuna baadhi ya watu tumewapa Uraia lakini matendo yao yanachafua hali ya usalama wetu,miongoni mwenu kunawanaojihusisha na wizi,uhalifu wa kutumia silaha,kuhifadhi waovu na kufanya vitendo vya kibaguzi kwa misingi ya maeneo mnayotoka.
Mbaya zaidi,kunawakimbi waliopewa uraia hapa nchi wanawatenga watanzania kwamba hawawezi kushirikiana nao.Natoa onyo kwa wote wanaofanya vitendo vya kibaguzi na kihalifu,Tanzania inaishi kwenye misingi ya Umoja,mshikamano na Ushirikiano wa hali ya juu bila kubaguana.Hivyo hatutakuwa tayari kwa watu wachache kuleta tabia mbovu ambazo hatujawahi kuziishi na tunaomba kila siku tusije kuziishi."anasema mwigulu.
Picha/Maelezo na Sanga Festo Jr.