Monday 18 November 2013

PICHA:VIONGOZI WA KITAIFA NA VYAMA VYA SIASA WALIPOSHIRIKI IBADA YA MAZISHI YA MAREHEMU DR.SENGONDO MVUNGI HII LEO


 Mh James Mbatia(MB) Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi akitoa neno la Shukrani kwa Watanzania na Wananchi wote waliojitokeza kufanikisha Shughuli ya Mazishi ya Marehemu Dr.Mvungi.Katika Hotuba yake Mh.Mbatia ameomba na kusisitiza sana serikali iimarishe ulinzi kwa gharama yeyote ile,Serikali ichukue hatua madhubuti kupambana na watu wanaojihususisha na vitendo vya kinyama kama hiki alichofanyiwa Marehemu Mvungi cha kuvamiwa na kukatwa Mapanga na kupelekea kifo chake.
 Watoto wa Marehemu Dr.Edmund Sengondo Mvungi wakitoa neno la shukrani kwa waombolezaji wote walojitokeza kwenye mazishi ya Baba yao,pamoja na namna serikali na viongozi wa NCCR walivyopambana kuokoa Uhai wa Baba yao bila Mafanikio.Kubwa Watoto wameahidi kuwa Watasoma sana kama Baba yao alivyosoma na kuwa msaada kwa taifa.
 Mh.Mwigulu Nchemba(MB) na Naibu katibu Mkuu wa  CCM Tanzania Bara akitoa shukrani za rambirambi akimuwakilisha Katibu Mkuu wa CCM Kanali Mstaafu Abrahaman Kinana,Katika Salamu zake,Mwigulu Nchemba amewasihi waombolezaji na watanzania kukemea na kuombea Taifa lisipatwe zaidi na huyu pepo wa mauaji anayeendelea kulikumba Taifa.Amesisitiza kuwa Serikali haiwezi kuwa sehemu yote ya nchi hii kwa muda wote,kikuwa ni ushirikiano wa Wananchi na vyombo vya Usalama kufichua mitandano hii ya unyama na mauaji.Mwigulu amesisitiza kuwa Taifa linapatwa na mikasa hii kwasababu watu hawana hofu ya Mungu,hivyo ni wakati wa kuamka kama Taifa na kushikamana kuombea taifa letu na kufichua maovu.
 Mh.Steven Masatu Wassira akitoa salamu za rambirambi kutoka Ofisi ya Rais,ambapo Mh.Wassira alisema Rais kikwete anatoa pole sana kwa familia na Watanzania wote kwa tukio hili ya kuondokewa na mtu muhimu sana kwa nchi yetu hasa kwa Mchakato mzima wa Mabadiriko ya katiba unaoendelea.
 Mh.waziri Mkuu Mizengo Peter Pinda akitoa Salamu za rambirambi kwa familia ya Marehemu Dr.Sengondo Mvungi,Kubwa alilozungumza Mh.Pinda ni kuwaomba watanzania kujiepusha na matendo maovu haya ya kuua watu wasio na hatia.Ameahidi serikali itafanya kazi yake kuhakikisha wahusika wanafikishwa sehemu husika na wanapata kuvuna dhambi walioipanda.Pia amewasihi Watanzania kumuombea Marehemu Mvungi huko aliko apokelewe na Bwana.
 Waziri Mkuu Mstaafu Jaji Warioba akitoa Salamu za rambirambi kwa waombolezaji na kumuelezea namna Marehemu Edmund Sengondo Mvungi alivyokuwa na msaada mkubwa kwneye mchakato wa katiba Mpya,Namna Mvungi alivyotanguliza Utaifa mbele na kauchana na ushabiki wa Chama.Mh.Warioba amesema anamuomba sana mungu waikamilishe kazi waliyotumwa na taifa hili(Katiba mpya) kwa amani licha ya kupata pigo kubwa la kuondokewa na kiungo muhimu sana kwenye mchakato mzima wa mabadiriko ya Katiba.
 Askofu kwa Kaskazini akilisha neno la Mungu waombolezaji wakati wa Ibada ya kuuga Mwili wa Marehemu Sengondo Mvungi.Askofu ameiomba sana serikali na Watanzania kuacha kabisa kufanyiana unyama wa namna alivyofanyiwa Mvungi kwakuwa mshahara wa dhambi niMauti.Na zaidi amesisitiza kuwa kila kiongozi,mwanasiasa na mtanzani mmojammoja ajitazame njia zake kwa namna anavyoishi na anavyolisaidia Taifa lake lisipatwe nda hii taibia ya watu kuuana na mmomonyoko wa maadili kwa vijana wetu.
 Mh.Mwigulu Nchemba akikabidhi rambirambi ya CHAMA CHA MAPINDUZI kwa mmoja wa wanafamilia wa Marehemu Edmund Sengondo Mvungi mbele ya waombolezaji.Rambirambi imetolewa na chama cha mapinduzi.
 Baba Askofu akiweka Shada la Maua kwenye jeneza lililobeba Mwili wa Marehemu Dr.Edmund Sengondo Mvungi.
Mh.Maghembe(kushoto) Mbunge wa Jimbo la Mwanga jimbo alilozaliwa Marehemu Mvungi akisikiliza kwa makini mafundisho ya Baba Askofu,.Huku(Kulia) Mh.Mwigulu Nchemba akiwa na uso wa huzuni kwa kumpoteza msomi mwenzake,Mwanasiasa Mwenzake Marehemu Edmund Sengondo Mvungi.
 

Mh.Mwigulu Nchemba Mbunge wa Iramba Magharibi na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Tanzania Bara akitoa Heshima za mwisho kwa Mwili wa Marehemu Dr.Edmund Sengondo Adrian Mvungi wakati wa Ibada ya mazishi iliyofanyika Parish ya Kisangara Juu wilaya ya Mwanga.
R.I.P DR.EDMUND SENGONDO ADRIAN MVUNGI

3 comments:

  1. Nikiwa mmoja wapo wa wana Kilimanjaro, nawashukuru watu wote na serikali ya ccm kwa jinsi mlivyojitokea kupitia waziri Mkuu, wamaziri wote, tume ya katiba na Mhe. Mwigulu Mnchemba aliyekuwa pamoja nasi kwenye msiba huo Vujini, Kisangara Juu.. Mch. Palemo Massawe

    ReplyDelete
  2. NIwashukuru wote hasa Mhe. Mwigulu Mchemba kwa kazi kubwa waliyofanya kusaidia kumpumzisha ndugu yetu hayat, Dr. Mvungi

    ReplyDelete
  3. Mh Kiongozi wa Upizani Kwenye Bunge la Jamuhuri ya Tanzania alikuwepo? kama alikuwepo mbona picha zake hazionekani; na alizungumza kabla yako; na kama wewe ndio ulikuwa mpiga picha basi ungempiga;Nisingeshangaa kutokuiona picha yako kama wewe ndio ulikuwa mpiga picha;Naomba maelezo'Au uchama nao;ulikuwa mbele kuliko utanzania; au kombati zake hazikuvutia kumpiga picha?

    ReplyDelete