Sunday 14 June 2015

MWIGULU NCHEMBA ATUA MKOA WA SIMIYU,APATA WADHAMINI KUELEKEA KUTEULIWA NAFASI YA URAIS NDANI YA CCM

Mwigulu Nchemba akiwasili Mkoa wa SIMIYU,Wilaya ya Itilima kwaajili ya kutafuta wadhamini wa nafasi ya Urais ndani ya chama cha Mapinduzi.Ndugu Mwigulu Nchemba akikabidhiwa orodha ya wanachama wa CCM waliomdhamini kwenye mchakato wa kugombea nafasi ya Urais ndani ya Chama.Anayekabidhi ni Katibu wa CCM ,Wilaya ya Itilima.Ndugu Mwigulu Nchemba akionesha fomu zilizojazwa na wadhamini wa wilaya ya Itilima ambao ni WanaCCM hai na waliohakikiwa na katibu wilaya wa Chama.Mwigulu Nchemba akitoa neno la Shukrani kwa wanaCCM waliomdhamini kwenye hii safari yake ya kuelekea Kugombea nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.Mh.Mwigulu Nchemba akiagana na Wananchi wa Itilima mara baada ya kukamilisha zoezi la kupata wadhamini ndani ya Mkoa wa Simiyu hii leo tar.14/06/2015.
"WAKATI NI SASA,MABADILIKO KWA VITENDO"

No comments:

Post a Comment