Tuesday 26 November 2013

KINANA AIJIA JUU SERIKALI,AITAKA IACHE URASIMU NA UMANGIMEZA KATIKA MIPANGO YA MAENDELEO YA WANANCHI.


  Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kujenga moja ya nyumba ya waalimu katika shule ya sekondari ya Ikuti iliopo katika kata ya Ikuti,Wilayani Rungwe Mkoani Mbeya mapema leo,akiwa sambamba na Ujumbe wake hawapo pichan,Katibu wa NEC,Itikadi na Uenezi Nape Nnauye pamoja na Katibu wa NEC,Siasa na Mahusiano ya Kimataifa,Asharose Migiro.Kinana na Ujumbe wake wako ziarani Wilayani Rungwe Magharibi mkoani Mbeya,ambapo kesho watakuwa wilaya ya Ileje kutekeleza Ilani ya chama,kukagua miradi ya chama na wanachi sambamba na kujua na kutatua matatizo yao kwa namna moja ama nyingine.
Wakienda kukagua moja ya bweni la kulala wanafunzi wa shule hiyo ya Ikuti
Katibu wa NEC,Siasa na Mahusiano ya Kimataifa ,Asharose Migiro wakielekea kuonana na balozi balozi wa shina la Kitonga,ndani ya kijiji cha Ikuti,Bwa.James Mbasi ,pichani nyuma anaefuatia ni Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnaupe
Katibu Mkuu wa CCM,pili kushoto,Ndugu Abdulrahman Kinana na wajumbe wake  wakielekea kuonana na balozi wa shina la Kitonga,ndani ya kijiji cha Ikuti,Wilayani Rungwe mapema leo.
Pichani ni Katibu Mkuu wa CCM pichani kati,Ndugu Abdulrahman Kinana akikata utepe kuashiria uzinduzi wa mradi wa kituo cha kuzalisha umeme kilichopo kwenye zahati ya Ikuti,katika kijiji cha Ikuti wilayani Rungwe mkoani Mbeya.

Kada maarufu wa CCM,Richard Kasesela akipiga ngoma ya asili ya kinyakyusa iitwayo Lipenenga.
Baadhi ya vijana mbalimbali wakiwa juu ya miti wakifuatilia mkutano wa hadhara,wakati Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana alipokuwa akihutubia jioni ya leo kwenye kijiji cha Ikuti.
Katibu wa NEC,Siasa na Mahusiano ya kimataifa,Asharose Migiro akizungumzaa mbele ya wakazi wa kijiji cha Ikuti mapema leo.
 Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnaupeakizungumzaa mbele ya wakazi wa kijiji cha Ikuti mapema leo,Wilayani Rungwe.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akizungumza na wakazi wa kijiji cha Ikuti mapema leo,kwenye mkutano wake wa hadhara .
Mbunge wa viti maalum mkoa wa Mbeya,Dkt Mary Mwanjelwa akifafanua jambo kwa wakazi wa kijiji cha Ikuti mapema leo,Mbunge huyo pia aliwataka akina mama kujiunga katika vikundi vya ujasiliamali,ili kurahisishiwa kupata mikopo ya kuendeleza miradi yao ambayo wataianzisha katika suala zima la kujikwamua na ugumu wa maisha,
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akizungumza na wafanyabiashara wa ndizi katika soko la Iponjora,Wilayani Rungwe,Kinana aliwaasa wafanyabiashara hao kutokuwa na tamaa ya kuuza biashara yao hiyo ya ndizi kwa bei ya kutupa,badala yake waachane na watu wa kati,wafanye biashara yao kwa faida na si kuwanufaisha wafanyabiashara wakubwa,ambao hawajui ugumu wa kilimo cha zao hilo,Kinana katika kuwaongezea kasi ya biashara yao ya ndizi aliwachangia kiasi cha shilingi laki moja
Katibu NEC,Siasa na Mahusiano ya kimataifa,Dkt Asharose Migiro akizungumza na wafanyabiashara wa ndizi katika soko la Iponjora,Wilayani Rungwe,mkoani Mbeya.
Wakazi wa kijiji cha Ikuti wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana na Ujumbe mara baada ya kuusimamisha msafara wake.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akizungumza na wakazi wa kijiji cha Lupando,Kata ya Masoko Wilayani Rungwe mapema leo,Kinana alizungumza mambo mbalimbali ikiwemo namna ya kutatua tatizo sugu la Maji na Barabara katika kijiji hicho,alichozaliwa Mbunge wa jimbo la Rungwe Magharibi,Mh.Dkt David Mwakyusa.Aidha kinana aliitahadharisha Serikali katika suala zima la kuitaka Serikali iache urasimu na umangimeza katika mipango ya maendeleo kwa Wananchi,kwa sababu Urasimu na umangimeza huo huwanufaisha zaidi wanaoshikilia fedha za miradi hiyo wakati wananchi Wanaumia na kuteseka kwa kukosa huduma muhimu mbalimbali.
Mbunge wa jimbo la Rungwe Magharibi,Mh.Dkt David Mwakyusa,akizungumza na wakazi wa kijiji cha Lupando,Kata ya Masoko Wilayani Rungwe mapema leo kuhusiana na kero mbalimbali zinazowatatiza wakazi hao,ikiwemo suala la maji na barabara sambamba na tatizo la bei ya zao la ndizi kutoka kwa wakalima kwenda kwa wafanyabiashara.
Mbunge wa jimbo la Rungwe Magharibi,Mh.Dkt David Mwakyusa akisalimiaa na Katibu NEC,Siasa na Mahusiano ya Nje,Dkt Asharose Migiro mara baada ya kukutana katika kijiji cha Lupango,Wilayani  Rungwe,ambapo Ndugu Kinana aliwahutubia wakazi wa kijiji hicho.
 Pichani shoto ni Mbunge wa viti maalum mkoa wa Mbeya,Dkt Mary Mwanjelwa akiwa na Katibu NEC,Siasa na Mahusiano ya kimataifa,Dkt Asharose Migiro walipokuwa wakielekea kukagua jengo la bweni la kulala wanafunzi wa shule ya sekondari ya Ikuti,Wiayani Rungwe mkoani mbeya leo.

 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akizungumza na wakereketwa wa shina la vijana waendesha boda boda katika soko la Kiwira,ambapo Ndugu Kinana aliwachangia kiasi cha fedha shilingi milioni tano kwa ajili ya kujiendeleza na kuwapa uwezo wa kujikopesha wenyewe katika suala zima la kujikwamua na suala zima la umasikini,hasa ikifahamika kuwa tatizo la ajira kwa vijana limekuwa kubwa.
 Pichani shoto ni Mbunge wa viti maalum mkoa wa Mbeya,Dkt Mary Mwanjelwa akiwa amepozi na mdau.

No comments:

Post a Comment