Thursday 13 February 2014

NAIBU KATIBU MKUU CCM,MH:MWIGULU NCHEMBA AKUTANA NA MGOMBEA UBUNGE (CCM)JIMBO LA KALENGA. Ndug.GODFREY WILLIAM MGIMWA

Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Tanzania-Bara Mh:Mwigulu Lameck Nchemba jioni ya leo Tar.13.02/2014 amekutana na Mgombea Ubunge Wa Chama Cha Mapinduzi Jimbo La Kalenga Mkoani Iringa Ndugu Godfrey William Mgimwa.Mh:Mwigulu Nchemba ambaye amekuwa akiongoza Mapambano ya Chaguzi Mbalimbali Nchini kwa Chama Cha Mapinduzi amempongeza Ndugu Godfrey Mgimwa Kwa Kuteuliwa Kwake Kuwa Mgombe Ubunge Jimbo la Kalenga"Wewe ni Kijana,Msomi tena Mchumi Kama mimi,Chama kimekuamini Sana kuwa wewe ndiye utakayepeperusha Bendera kwenye Jimbo la Kalenga,Hongera sana,Nakuahidi kushirikiana Mwanzo hadi Mwisho kuhakikisha Kalenga inabaki Salama Mikononi Mwa Chama Cha Mapinduzi" .

No comments:

Post a Comment