Thursday 20 February 2014

PICHA:MH:MWIGULU NCHEMBA AFUNGUA SOKO LA WAKULIMA "OLD KIOMBOI",LIMEJENGWA KWA NGUVU YA WANANCHI,MBUNGE NA TASAF TWO

Mh:Mwigulu Nchemba Mbunge wa Iramba akikata Utepe Kufungua Soko la Wananchi Wa Old Kiomboi hii leo alipofanya ziara ya kukagua Maendeleo Jimboni Kwake na Kuzungumza na Wananchi mapema hii leo 20/02/2014.
 Soko hili limejengwa kwa Nguvu za Wananchi,TASAF na Mchango Binafsi wa Mh.Mwigulu Nchemba wa zaidi ya Milioni 10 za Kitanzania.Soko hadi kukamilika kwake kama Jengo,Meza na Vyoo limegharimu Tsh.Milioni 85.
 Sehemu ya Meza zilizotengenezwa kwa kusakafiwa na Cement ndani ya Soko hili la Old Kiomboi.
Upande wa Mbele wa Soko la Old Kiomboi.
 Mbunge wa Iramba Mh.Mwigulu Nchemba akitembelea wafanyabiashara walioanza kuuza Bidhaa zao ndani ya Soko la Old Kiomboi.
Mh.Mwigulu Lameck Nchemba,Naibu Waziri wa Fedha akizungumza na Wananchi wa Old Kiomboi mara baada ya Kuzuindua Soko walilojenga Wananchi kwa Nguvu zao wakichangiwa na TASAF TWO Pamoja na Mbunge wao.
Mh.Mwigulu Nchemba amewasifu Wananchi kwa kuunganisha Nguvu zao na hatimaye kujenga Soko,Pia amewaomba kuwa walitumie soko hilo kwa Ushirikiano Mzuri wa wao kwa wao,Kujenga Jengo na Kuacha kulitumia si Jambo jema kabisa kabisa.Mh.Mwigulu Nchemba amesema"Naiomba serikali na wote wanaohusika na Ukusanyaji wa Kodi waangalie Viwango vya Ukusanyaji Kodi kwa Wafanyabiashara wa soko hilo,Isije kuwa kunakuwa na Makato ya Jumla bila kutofautisha mitaji ya Wafanyabiashara,haki itendeke kukusanya kodi kutokana na Kiwango cha Biashara cha Mtu".
Mbali na hilo Mh.Mwigulu amewataka Kamati ya Wananchi ilihohusika kwenye Ujenzi wa Soko hilo,Kuhakikisha wanafanya utafiti wa Gharama za Umeme unaotakiwa Kuwekwa kwenye Soko hilo,Yeye kama Mbunge wa Iramba anachukua Jukumu la Kusimamia na kuhakikisha Umeme unawaka kwenye Soko hilo ilikuwapa nafasi Wafanyabiashara kufanya shughuli zao hata Nyakati za Usiku. 
Hili ni Soko Kubwa la Pili kuzinduliwa Eneo la Kiomboi,Mwaka jana wakati wa Mbio za Mwenge.Mh.Mwigulu Nchemba pia alishiriki Uzinduzi wa Soko la Misigiri la Wakulima.Soko lenye Ukubwa sawa na hili la Kiomboi.

No comments:

Post a Comment