Thursday 20 February 2014

TASWIRA:MH:MWIGULU NCHEMBA AMEFANYA MKUTANO MKUBWA KIOMBOI-IRAMBA,"SERA/SHERIA YA MANUNUZI SERIKALINI NI MZIGO KWA SERIKALI",AAGIZA WASIO SOMA MAPATO NA MATUMIZI WACHUKULIWE HATUA ZA KISHERIA

Mh:Mwigulu Nchemba akisalimiana na aliyekuwa Mbunge wa Iramba Mwaka 2005-2010  ambaye kwa sasa ni MNEC-CCM wa Iramba.
 Mh.Mwigulu Nchemba,Naibu waziri wa Fedha kiwa Meza Kuu tayari kwenye Eneo la Mkutano Viwanja vya Stand ya Kiomboi Jimboni Kwake Iramba,
Naibu Katibu Mkuu CCM-Bara Mh;Mwigulu Nchemba akisalimiana na Wananchi wa Iramba waliofika Viwanja Vya Stendi ya Kiomboi kwaajili ya Mkutano wa Hadhara wa Mwigulu wa kuzungumza na Wananchi kuhusu Miradi ya Maendeleo Mbalimbali pia Kusikiliza Kero zinazowakumba Wananchi wake ndani ya Jimbo la Iramba.
 Sehemu ya Mamia ya Wananchi waliofika Kwneye Mkutano Wa hadhara wa Mh;Mwigulu Nchemba hapa Kiomboi hii leo 20/02/2014.
Mh;Mwigulu Nchemba Mbunge wa Iramba akizungumza na Wananchi wake hii Leo Viwanja vya Stendi Kiomboi.
 Na.Mwandishi Wetu.
Mbunge wa Iramba Mh;Mwigulu Lameck Nchemba,Naibu Waziri wa Fedha na Naibu Katibu Mkuu CCM-Bara hii leo 20/02/2014 amefanya Mkutano wa hadhara Makao Makuu ya Wilaya ya Iramba,Viwanja Vya stendi ya Kiomboi kuzungumza na Wananchi wake kuhusu Miradi ya Maendeleo ndani ya Jimbo lake na Kero kutoka kwa Wananchi.
Akizungumza na Wananchi wa Iramba,Mh:Mwigulu Nchemba amesisitiza kuhusu Matumizi na Utunzani Mzuri wa Fedha za Umma"NImekuja hapa kutoa mrejesho wa shughuli mbalimbali za Maendeleo zinazofanyika ndani ya Kata zetu/Jimbo letu,Lakini Kubwa lililonileta ni kuhusu Mahesabu na Utunzaji wa Fedha za Umma.Kumekuwa na tabia ya Watumishi wa Serikali kukalia Kusoma Mapato na Matumizi kwa Wananchi wao,Hili ni Jambo lisilokubalika Kabisa Kabisa,Viongozi wa serikali wanaojua Wajibu Wao ni Lazima waweke wazi Mapato na Matumizi kwa Wananchi wao."Amesema Mwigulu.
Mh:Naibu Waziri akaongeza kwa kusema"Naagiza kwa Mkuu wa Wilaya,Hili ni agizo na sio Ombi,Naomba awachukulie hatua kali sana Viongozi wote waliokalia Kusoma Mapato na Matumizi kwa Wananchi wao,hakikisha unafuatilia fedha za miradi zote zilizopelekwa kwenye kila kata.Mimi Kama Mbunge wenu hadi sasa kila kata ya Jimbo hili nimeshapeleka zaidi ya Miloni 3 kwa kila kata kwaajili ya Kusaidia Shughuli za Maendeleo.Naagiza Mkuu wa WIlaya kufauatilia fedha hizo,pamoja na fedha zingine za Maendeleo kuhakikisha zimefanya kazi iliyokusudiwa.Kwa yeyote mwenye taarifa kuhusu Kiongozi wa serikali kutumia vibaya Fedha za Umma naomba atoe taarifa kwa Mkuu wa WIlaya au Ofisi yangu ili Sheria stahiki zichukuliwe."

Mbali na hapo Mh;Mwigulu Nchemba ametoa Ambulanche Moja kwaajili ya Wananchi wa Kata ya Shelui,Pia ametengeneza Ambulance ya Kata ya Ndago na imeshapelekwa Hospital ya Ndago kwaajili ya kusaidia Wagonjwa.Mbali na huduma hiyo ya Kiafya,Mh:Mwigulu Nchemba ameshaorodhesha Vijiji mbalimbali vya kata zote kwenye Mpango wa Kupitisha Umme,Kuna Vijiji kata ya Ndago vimeshawashwa Umme.Kazi ya Kuweka Nguzo za Umme kwenye Vijiji vilivyopo kwenye mpango wa Umme mwaka 2014/2015 imeshaanza.

Pia Mh:Mwigulu Nchemba ametumia Mkutano huu kuwaeleza Wananchi kuwa,Ameamua kulivalia Njuga swala la Sera ya Manunuzi Serikalini.Sera ya Manunuzi imekuwa ikiipa Serikali Mzigo mzito sana,Kwani Wazabuni wengi wamekuwa wakitumia Mwanya huo kujipatia Fedha Nyingi tofauti na uhalisia wa huduma inayotoelewa.Mh;Mwigulu Nchemba ametolea mfano kuwa,Duka lile lile mtu wa kawaida ananunua Soksi kwa TSh.1000,lakini Duka lile lile Kupitia Mzabuni wa Serikali Soksi Zile zile zinanunuliwa kwa Tsh. 7000.Hivyo Serikali inapoteza Fedha nyingi sana kwenye Manunuzi ambayo Sheria yake haijawa na Faida kwa Serikali zaidi ya kuwa mzigo.

No comments:

Post a Comment