Wednesday 13 August 2014

VIDEO.. MWIGULU AKAMATA WAHUJUMU UCHUMI WALIOKUBUHU NCHINI.


Mh:Mwigulu Nchemba Naibu waziri wa Fedha akimbana kwa Maswali mtuhumiwa wa Kuhujumu Uchumi wa Nchi na kukwepa Kodi Bwana Fayaz Nassoro wa CI GROUP.
Mtuhumiwa huyu anadaiwa Kukwepa kodi kwa Zaidi ya Bilioni 7 za Kitanzania kuanzia mwaka 2009 hadi 2013.Pia ametumia Mashine Feki ya EFD kuzalisaha risiti Feki kwa Makampuni ya VodACOM,Tigo,TBL katika hatua za kudai Marejesho Serikalini hivyo kuliingizia Taifa hasara. Mmoja ya Watuhumiwa wa Uhujumu Uchumi walionaswa na Mh.Mwigulu Nchemba.

4 comments:

  1. Absolutely Brilliant, Keep it Up, Save our Nation!

    ReplyDelete
  2. CI Group ni kampuni ya kijanja sana. ..huyo mama anajidai kujitia rafiki wa mama Rais. .

    ReplyDelete
  3. Mheshimiwa Naibu Waziri, pamoja na Watanzania wote wenye mapenzi mema na wenye uchungu na rasilimali za Tanzania! Kwanza nakupongeza Mheshimiwa Mwigulu Nchemba kwa ujasiri wako, uzalendo, na pia kujivunia kuwa Mtanzania kuwanasa hawa wahujumu uchumi. Wamekuwa na mazoea ya kuwanyanyasa hata waajiriwa wao mimi nikiwa mmojawao kwani niliwatumikia kupitia kampuni yao tanzu (Media Holdings Ltd. baadaye ikabadilishwa na kuwa Media Express Ltd.) kwa muda wa miaka 12 lakini wakanilipa "Gratuity" ya shilingi za kitanzania 1,150,000/= (Milioni moja laki moja na nusu tu) na sikulipiwa NSSF, wala P.A.Y.E. kwa miaka yote hiyo 12. Ninayo mengi sana ya kuelezea .....lakini za mwizi ni 40.

    ReplyDelete
  4. Kaka unajua huyu Fayaz kampuni sio yake ameajiriwa tu na mhindi mwenziye, Sasa mmefikia wapi maana kimya kingi, na watu wako mtaani wanaendelea kupiga kazi kama kawa

    ReplyDelete