Wednesday 2 September 2015

MWIGULU NCHEMBA AKUTANA NA WANANCHI WA BABATI,AHOJI UHALALI WA UKAWA KUNUKUU MANENO YA BABA WA TAIFA WAKATI WAMEPOTOKA

Mwigulu Nchemba akiwasili eneo la Mkutano nje kidogo na Mji wa Babati hii leo alipofika kwaajili ya Mkutano wa kampeni wa kuinadi Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya Mwaka 2015.Pia kuwanadi wagombea Udiwani na Ubunge kwa Babati Mjini.Kutoka Kushoto ni Katibu wa CCM Mkoa wa Manyara Ndg.Ndekubali,Katikani ni Mwigulu Nchemba na Mwisho kulia ni Mh.Chambili ambaye ni Mgombea Ubunge Jimbo la Babati Mjini.Mwigulu Nchemba akisalimiana na Wananchi wa Babati hii leo,Katika hotuba yake amesisitiza Wananchi waachane na maigizo yanayofanywa na baadhi ya wagombea Urais bali waamue moja la Kuchagua Rais Mchapa Kazi,.Mweigulu amesisitiza Zaidi kuwa rekodi za wagombea Urais zipo wazi kila kona na kwa rika zote.Hivyo watanzania watumie fursa hii kuhakikisha Taifa linapata kiongozi Mchapa kazi ambaye ni J.Pombe Magufuli wa CCM.Sehemu ya mamia ya Wananchi waliofika kusikiliza Ilani ya chama cha Mapinduzi wakishangilia namna Ilani ya chama hicho ilivyoweka bayana namna ya Kutekekeleza shughuli za maendeleo katika Jimbo la Babati Mjini,Mh.Mwigulu Nchemba akiwa na Mgombea Ubunge Jimbo la Babati Mjini Ndg.chambili wakiagana na Wananchi mara baada ya Mkutano huo wa kampeni wa CCM."CCM ni Ile Ile"
Picha na Sanga Jr.

No comments:

Post a Comment