Wednesday 5 February 2014

NAIBU WAZIRI WA FEDHA MH:MWIGULU NCHEMBA AKUTANA NA WATENDAJI TRA MKOANI MBEYA,ATOA MSIMAMO MATUMIZI YA MASHINE ZA EFD

Naibu Waziri wa Fedha(sera) Mh:Mwigulu Lameck Nchemba akiwa katika picha ya pamoja na Wafanyakazi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoani Mbeya mapema hii leo.
 Naibu Waziri wa Fedha Mh:Mwigulu Nchemba akiwasili Ofisi za Mamlaka ya Mapato TRA Mkoani Mbeya hii leo wakati wa Ziara yake ya Kikazi ya kutembelea Ofisi zote za TRA,Ofisi za Hazina ndogo na Kuzungumza na Wafanyabiashara katika Mikoa ya Njombe,Ruvuma na Sasa Mbeya.
Naibu Waziri wa Fedha Mh:Mwigulu Nchemba akizungumza na Watendaji/watumishi wa TRA,Hazina ndogo,Takwimu na Uhakiki Mali Mkoani Mbeya mapema hii leo asubuhi.

Na,Habari Kwanza Blog.
Naibu Waziri wa Fedha (Sera) Mh;Mwigulu Nchemba hii leo asubuhi (Tar.05/02/2014)  amekutana na Watendaji/Watumishi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA),Hazina Ndogo na Wahakiki Mali za Serikali Mkoani Mbeya Kwaajili ya Kufahamiana nao,pia Kuzungumza nao kuhusu Uboreshaji wa Ukusanyaji wa Mapato Nchini,Msimamo wa Serikali kuhusu Matumizi ya Mashine za EFD kwenye Ulipaji kodi,Pia Uadilifu na Ushirikiano katika Utumishi wa Umma hususani kwenye Wizara ya Fedha.
Akizungumza na Watendaji hao,Naibu Waziri amesema,Serikali imejipanga na itaendelea kusimamia zoezi la kuhakikisha Wafanyabiashara wanatumia mashine za EFD ilikukusanya kodi halisi ya bidhaa/huduma wanazotoa kwa Wananchi.Utumiaji wa mashine za EFD kwa wafanyabiashara unaboresha kipato halisi cha bidhaa wanazoziuza,pia mashine zinasaidia kudhibiti mianya ya Ukwepaji wa kulipa kodi Nchini.
Kwa Mkoa wa Mbeya wenye Wafanyabiashara walipa kodi waliojiandikisha 32647, kuna zaidi ya Wafanyabiashara 297 walionunua mashine za EFD na zaidi ya 300 wameshaanza kulipa kwa awamu iliwaweze kupatiwa mashine hizo,Idadi hii ya wanunuzi wa Mashine za EFD imeongezeka kwa kasi mara baada ya Mgomo wa Wafanyabiashara uliofanyika 1/10/2013 kupinga matumizi ya Mashine hizo.TRA kupitia mawakala wake wamekuwa wakitoa Elimu ya Matumizi ya mashine hizo kwa wafanyabiashara na hatimaye uelewa umekuwa mkubwa na sasa wengi wamejitokeza kununua mashine hizo.
Pia Mh:Mwigulu Nchemba amesisitiza Ushirikiano na Umoja kwenye Utumishi wa Ofisi za Umma hususani hizi za Ukusanyaji wa kodi Nchini.Haikubaliki kwa Mtendaji/mtumishi wa TRA na idara husika za mapato kufanya ubadhirifu wa kodi za Watanzania wakati serikali inatumia nguvu kubwa kuhakikisha kodi Inakusanywa kwenye vyanzo vyote.Ni wajibu kwa kila Mtumishi kufuata sheria za Nchi  za Utumishi ilikuondokana na adha atakayoipata pindi Ofisi yake ikibaini kuna watendaji wanaofanya ubadhirifu wa kodi za Watanzania.

No comments:

Post a Comment