Tuesday 4 February 2014

PICHA,MH: MWIGULU CHEMBA AKUTANA NA WAFANYABIASHARA WILAYA YA KYELA

Naibu Waziri wa Fedha akizungumza na Wafanyabiashara hii leo Wilayani Kyela kuhusu Matumizi ya Mashine za EFD na Umuhimu wa Kulipa kodi kwenye Biashara zao. 
Sehemu ya Wafanyabiashara wa Wilaya ya Kyela waliofika kwenye  Mkutano wa Mh;Mwigulu Nchemba Naibu Waziri wa Fedha(Sera) hii leo.
 Naibu Waziri wa Fedha Mh:Mwigulu Nchemba hii leo amekutana na Wafanyabiashara wa Wilaya ya Kyela katika mwendelezo wa ziara yake ya Kikazi ya kukutana na Watendaji wa Mamlaka ya Mapato(TRA),Wafanyabiashara na Watendaji wa Ukusanyaji wa Ushuru wa Forodha(mipakani).
Akizungumza na Wafanyabiashara wa Kyela,Mh:Mwigulu Nchemba amewatoa hofu wafanyabiashara kuhusu Matumizi ya Mashine za EFD kwenye Biashara zao,amesisitiza kuwa Kukosena kwa Elimu ya Kutosha kuhusu Mashine hizo kumepelekea Wafanyabiashara wengi kulalamika hata kabla ya Kununua mashine zenyewe.Mashine za EFD zimeidhinishwa na Mamlaka ya Mapato kutumika kwenye ununuzi wa bidhaa kwa wateja ilikudhibiti ulipaji wa kodi za bidhaa na huduma mbalimbali za kibiashara.
Mh:Mwigulu amewaeleza Wafanyabiashara wa kyela kuwa Mashine za EFD ni bora sana hasa kwa kukuza faida kwa Wafanyabiashara kupitia ulipaji Kodi usiokuwa na vikwazo.Amewaomba wananchi kununua mashine hizo kwa haraka sana na TRA imejipanga kutoa huduma kwa ukaribu zaidi kwa yeyote atakayekuwa na tatizo na mashine hizo za kukusanyia mapato ya kodi.
Pia Naibu Waziri wa Fedha ametaka Wakazi wa Kyela kaucha kutumia njia za panya kupitisha bidhaa zao,Kitendo cha kutumia vipenyo vya mto Songwe kukwepa kulipa Kodi ni kitendo cha kuhujumu Uchumi wa Nchi,Pia ni Kosa kisheria kuingiza bidhaa ya nje ya nchi bila idhini ya Serikali ya Tanzania kupitia Idara zake za Ushuru wa Forodha.Hivyo ni muhimu kuachana na mchezo huo wa kuhujumu Uchumi,Serikali ya Tanzania na Malawi zimejipanga kuhakikisha ushuru wa Forodha na kodi mpakani utakuwa unakusanywa kwa Kituo Kimoja cha pamoja(One-Stop Border Post) ilikurahizisha upitishaji wa Mizigo mpakani Mwanchi hizi mbili.
Mbali na hapo,Serikali inachukua hatua za kuangalia namna ya kuhakikisha bidhaa zinazovushwa kwa magendo(Sukari n.k) zisizo na athari kwa Watanzania zitatafutiwa namna ya kupatikana kwa Wingi ilikuondokana na uingizaji wa Bidhaa kwa njia za Magendo.

Vilevile Soko la Mchele linatafutiwa dawa ya Kudumu kwa Wafanyabiashara wote,Serikali imesikia kilio cha wauzaji wa mchele hasa kitendo cha kuingiza  Mchele wa nje ya Nchi na kusababisha soko la Mchele wa ndani kuwa gumu kwa Watanzania wenzetu.
Awali Mbunge wa Kyela Mh:Waziri wa Uchukuzi Harrison Mwakyembe akizungumza na Watendaji wa Halmashauri ya Kyela,TRA na Watumishi wengine alisema "Nimeshangwaza sana na Wafanyabiashara kukataa kutumia mashine za EFD wakati ndio mkombozi wa baisharazao na Ulipaji Kodi kwa Nchi yao.Nimeshangazwa zaidi hata wauza maandazi,Machinga wa barabarani,Wauzaji wa Viatu wanaotembeza nao wanalalamika mashine za EFD wakati wao haziwahusu kabisa kabisa,Naomba TRA watoe elimu ya Kutosha,Wafanyabishara wengi wanarubiniwa,kudanganywa na Watu wachache kuhusu Mashine za EFD za kukusanyia mapato kwa sababu Wachache hao ni wale waliokubuhu kukwepa Kodi hapa Nchini.Hivyo Watanzania tumieni mashine za EFD kukuza Uchumi wa Nchi yetu kupitia mapato ya Kodi.
Chanzo:Habari Kwanza Blog

No comments:

Post a Comment